Tuesday, August 24, 2010

Habari za Miaka mingi? Nilienda kuoa sasa nimerudi

Thursday, June 26, 2008

Wakulima wetu!

Picha kwa hisani ya Charahani.
Nimepitia Blogu ya charahani leo nikakuta picha ya kuvutia sana.

Picha hii inaonyesha moja ya vijana wanajitahidi kujenga afya zetu kwa kutumia akili zao katika kilimo. inafurahisha sana kuona kwamba kuna vijana katika nchi hii wenye uwezo wa hali ya juu katika kilimo na kuzingatia wanaanzia bila mtaji wowote lakini wanafanikiwa kutunza bustani katika hali hii!
Hii inaonyesha jinsi tusivyohitaji wawekezaji toka nje katika sekta ya kilimo kama inavyosemwa na wachache kati yetu ikiwamo waheshimiwa wetu waliopo pale bungeni. Sijui hawa wanatoa wapi owoga walionao, nashangaa jinsi wasivyojiamini na kutodiriki kufanya uchunguzi wa kina ili watambue uwezo tulionao katika kilimo miongoni mwa vijana wa Tanzania. Naona hawa wachache bado hawajua faida ya kilimo kama biashara na kuainisha matatizo wanayopata wakulima wetu hata kushindwa kukiendeleza.
Ninasema kwa majigambo kuwa "wakulima" wetu wanafanya kazi kubwa sana na wanamafanikio mazuri sana ukiangalia mazingira wanayofanyia kazi, mitaji wanayoanza nayo na teknologia wanayotumia! kiasi wanachozalisha ni kikubwa sana na bado kuna uwezekano wa kuzalisha zaidi kama tunataka wafanye hivyo. Jana kwenye luninga wakulima wa mbinga walisema kwa mafunzo ya shamba darasa waliopata toka kwa mtaalamu wa kilimo katika wilaya yao wamefanikiwa kuzalisha kahawa nyingi kuliko walivyotegemea na walivyowahi kuzalisha.
Sijui kama hao wawekezaji katika kilimo watatoka kwa mungu, ambako hatuwezi kuhoji uwezo wao!, au watatoka bara jingine , ambao tukienda jifunza nao huwa tunaonyesha uwezo wa hali ya juu kuliko wao, ndio waje walete mapinduzi ya kilimo nchini mwetu! kichekesho kikubwa sana hiki.
Uwekezaji unaingia kwa kishindo katika kila sekta, sijui kama wananchi watapata nafasi huru ya kuwekeza katika sekta yeyote, tutaishia kushindana vita ya kushindwa na Bunge Ltd toka marekani wakati sisi tunanyimwa fursa ya kupata mitaji.
Sijui hizo sekta zinazopewa kipaumbele kama kusamehewa kodi kwa kipindi fulani, kutengewa maeneo maalumu na vituo maalumu vya kuwasaidia wanafaida gani kwetu kama kilimo kilivyo.
Sioni tutakachopoteza kama tunachopoteza kama hatutafanya chaguzi au tunavyofuga uzembe katika Tanesco, tukiweka pesa zetu kwenye kilimo ambacho ninakipa umuhimu wa hali ya juu kuliko sekta zote hapa nchini. Tunahitaji mapinduzi ya Kilimo kama tunataka maisha bora kwa kila mtanzania. Mapinduzi ya kilimo yatapatikana kwa njia zifuatazo;
-kuweka wananchi katika vikundi/ushirika wa kilimo
-kupatia hivi vikundi/ushirika uweza wa kukopa dhana za kisasa za kilimo
-kutoa mafunzo ya kilimo cha kisasa kwa vikundi/ushirika wa kilimo
-Kuhakikisha masoko yenye kutoa bei halali kwa mazao ya kilimo kama wafanyakazi wengine wanavyolipwa mishahara halali
-Kuhakikisha matendo ya ufisadi katika sekta ya kilimo yanakemewa kwa adhabu kali sana, hata kifo, kwa atakayepatikana na kosa la kuhujumu kilimo.

Hakuna Maisha bila kilimo.

Wednesday, January 23, 2008

NIMEPOTEZA MDOGO WANGU

Tarehe 17.01/2008 ilikuwa siku mbaya sana kwangu, baada ya kuwa na shaka ya siku tatu kuhusu hali ya mdogo wangu Majaheni T Newa nilipokea habari ya kusikitisha sana kuhusu kifo chake.Mazishi yalifanyika tarehe 19/01/2008.
Majonzi yaliyonikuta hapo sijui kama sio ndugu, jamaa na marafiki kunituliza yangenipeleka mahali ambapo hakuna ambaye angeamini.

Nashukuru wale walioshirikiana nami katika kipindi hicho kigumu na vilevile kuomba msamaha kwa wale ambao tukio hilo liliwagusa na tukashindwa kupatiana habari.

Sunday, August 05, 2007

Matapeli wa Kishairi - Lyrical Crooks

Come listen to me
I made a discovery
I wanna share it with you
I have you know that is true

Multi-nationals are really criminals
all forms of gambling
there is no way you can win
open your eyes guys
its time you realize
that the rise in price
is to make more money
for those who has got plenty
and the trick of the trade
is to keep the hungry be listen empty

It’s the break of the day
its time you have to say
you have been sleeping all night
now its time for the light
come see lyrical crooks
who have learn their tricks by the books
so come disciples of god
who rule with an iron rod

Mtunzi: Bob Andy
Wimbo: Check it out
Album: Retrospective

Bob Andy katika wimbo huu anatutahadharisha na watu anaowaita “lyrical crooks” akimaanisha “matapeli wa kishairi” waliojifunza utapeli kwa kutumia vitabu, inawezekana ni kitabu cha Shakespeare au kile chetu cha abunuwasi au hivi vya kisasa na kidini. Watu wa aina hii wako wengi sana hapa kwetu na kibaya zaidi ni wale tunaowaamini sana, wanafanya maamuzi yakutuumiza halafu wanakuja na mashairi yao mazuri waliotumia muda mrefu kuyatunga na kuyakariri wakituhadaa tukubaliane na maamuzi yao kwamba yatatusaidia wakijua mwishowe ni matatizo kwetu na sio kwao.
Ingawa ni wimbo wa zamani kidogo lakini mtunzi alishaliona hili jinamizi la utandawazi kwa kupitia mtangulizi wake “Multi-nationals”au makampuni ya kimataifa! yenye utaifa! Sijui hawa watu huwa wanafikiria nini kwa dude hili, kuendeleza nchi? Kujiendeleza? Au kuingiza majina yao kwenye vitabu vya historia ( His-Story) kwamba waliwasaidia kukuza mitaji ya wale wanyehaki ya kuimiliki dunia? Nikiutafakari huu Utandawazi, huwa nashindwa kujielewa, hivi almasi na dhahabu nyingi zilizochimbwa Shinyanga na watu wasiokuwa wa-Tanzania, zikapelekwa Japan/Malaysia kuchongwa na Baadae kuuzwa kwenye soko la London na mapato yake kuhifadhiwa kwenye benki ya Australia zitanyanyua uchumi au pato la Tanzania kuliko ile kidogokidogo na itakayoendelea kuwepo kwa muda mrefu sana, iliyochimbwa Shinyanga, na wa-Tanzania, kisha kupigwa mnada Dar es salaam, bila kujali inapelekwa wapi, kisha mapato yake kuwekwa kwenye benki ya NMB! Lazima mmoja wetu atakuwa anakichaa! Na anacheza kamari, kama karata tatu, ambayo huna uwezo wa kushinda.
Wanaendelea na utapeli wao wa kishairi, wanapandisha bei kwa mashairi mengi yanayotuambia kuwa wanatujali! Huku wanachukua kidogo kwa wasionacho na kwaongezea wenye kingi sana! Na kuendelea kutubembeleza tuwasikilize wakijua tumeshakata tamaa.
Siku mpya itaanza tuu, tutaamka toka usingizi tuliolala siku nyingi sana, jua likituangazia tupate usemi wa kuwaambia tukiongozwa na mtume toka kwa mungu mwenye kuongoza kwa kutumia mkono wa chuma

Tuesday, June 26, 2007

Hawa wana nini kwenye vichwa vyao?

Kila mara nasikiliza rege kupata ujumbe uliopo ndani yake. Na muda huu nikiandika nimevutiwa na kazi ya Bob Andy (pichani) yeye anaanza kwenye wimbo wake wa “Fire Burning” na swali hili
“ Would I have to ask you leaders what do you have in minds?”
Naona hili swali liko kwenye wakati muafaka kwenye kipindi hiki, Napenda kumuuliza Waziri Mama wa Fedha, Anafikiria nini kwenye akili yake kupanga bajeti kama ile aliyoisoma Juzi bungeni? Isitoshe makada karibu wote wa CCM wanaiunga kwa nguvu zote sijui nao wana njama gani na sisi wafanyakazi wa nchi hii, wote wana-CCM na wapinzani.
Bajeti hii inaelekeza kupandisha bei ya bidhaa zote zijulikanazo hapa Tanzania. Sijui katika hali hii ambayo kila mtu analia hali ngumu ya maisha mwingine anataka bei zizidi kupanda, bila kutupa mkakati unaoeleweka wa kuzikabili hizo bei.
Bob Andy ameendelea kutuambia,
“You are protesting on the wrong side of the fence”
“ read the lines on your fence you will be safe for sure’
Tumepiga makelele makali sana kuonyesha kutoridhika na hiyo bajeti, lakini ikapita kwa kishindo kikali sana, na mhariri wa gazeti la chama na kongwe zaidi aliweka habari ya juu kwamba Bajeti yapita kwa kishindo!, labda ni sisi ndiyo tuliipinga tukiwa tumekaa upande mbaya ambao makelele yetu hayakusikika! Au hatukusoma ishara kwenye kuta zetu tukajiingiza kwenye haya matatizo na sasa tunajua tukiwa tumechelewa!
Nikamkumbuka Mutabaruka katika shairi lake wa “Revolutionary Words” naye alisema,
“Revolutionary words have become Entertainment, Dramatizing the suffering of people in their revolutionary words”
hiki ndiyo kilichofanyika bungeni! Makelele yote waiopiga wabunge, hasa wa CCM, yalikuwa ni maigizo ya jinsi wananchi watakavyo hangaika na kulia na mzigo waliobebeshwa na bajeti hiyo. Walipochekesha Kiasi cha kutosha wakarudia kwenye kazi yao – kudai posho zao nono. Hesabu posho za siku moja walizopewa Taifa Stars utajua wanachukua ngapi kwa siku!
Linton Kwesi Johnson naye alishatuambia kwamba,
“The JLP, cyant set wi free,
the Liberate dem cyant do it fi wi,
make dem gwaan, now wi come,
wi haffi storm like a rising sun.”

Benjamin Zephaniah yeye alikataa kupewa tuzo ya OBE (amepewa Salman Rushdie juzi juzi akazua balaa kwenye jamii ya kiislamu) na malkia wa Uingereza sababu anaendelea kuunga mkono unyonywaji na ukandamizaji unaofanyika ulimwenguni.
Bado Bob Andy aliendelea kuwakumbushia kuwa,
“ Hell a go run loose, if you don’t delivering”
huu ujumbe uwafikie wanye kazi ya kupanga na kusimamia maendeleo ya Watanzania wakae vizuri kabla jehanamu haijajifungua hapa jirani, wajue maneno aliyoingia nayo JK ikulu na wajue tupo millioni na zaidi tunaotafuta nafasi ya kuyatekeleza kwa vitendo!
(picha zote kwa uhisani wa internet)

Friday, March 23, 2007

Bado Nipo

Habari za Mwaka mpya? Mambo mengi yamejitokeza tangu kuanza kwa mwaka huu, mengine yanakubalika na pia mengine hayakubaliki wali kutegemewa, licca ya hayo yote nilipotea kwa muda mrefu kidogo bila kutoa salaam zangu za mwaka mpya, ingawa nilipita kupokea zilizotolewa na wenzangu.
Kazi bado zinaendelea, Blog zinaongezeka na wanablog pia wanaongezeka. Yule jamaa wa annony... bado anasumbua! anaweka posting zake kwangu ambazo sijui nifanyie nini lakini we acha tuu! iko siku atakomeshwa.
Kipenzi cha afrika, Mugabe, ameingiwa na kasheshe nyingine, naona inafanana na ile iliyotokea Denmark lakini haikuwa "issue" kubwa sana kama anavyofanyiwa Mugabe ingawa hakuna mtu aliyekufa kama Denmark, Tunasimama naye na udhalimu utashindwa.
Nyumbani majambazi yamerudi tena wiki hizi zilizopita, lakini "sangoma" wao hana nguvu za kuishinda jamii, wote watatulizwa.
Sikujua kama watu huwa tunakamiana kiasi hiki bila sababu ya maana na za aibu kama madeni anayolalamika Vitali Maembe kuachiwa na kaka yake, .... kuberi dukani kwa mpemba, bangi kwa pusha jeda na gongo kwa mama ..... . Bado najifikiria hili lilikuwaje lakini nimeathiriwa na jambo hili hivyo nitaliongelea nikiwa na habari za uhakika.
Mambo yanabadilika, barabara iliyoliliwa siku nyingi, kilwa, imeanza kutengenezwa tunaomba isiwe nyembamba kama ile ya shekilango, naona sasa ndugu zetu akina baa wa ntwara watapata ahueni ya usafiri ingawa bado wana mshale wa nauli za juu unawangojea wao. Tuombe mwaka huu ubadilishe hali kidogo.
Tulipata ugeni wa kimataifa, maaskofu wa kianglikana walifanya mkutano hapa Tanzania, maazimio yao kidogo yalifanana na Watanzania, labda sababu hii ni nchi takatifu hata ukija na dhamira zako chafu hutaingia nazo! Nadhani na Umoja wa Mataifa nao uje fanya mikutano yao hapa pengine nao watafikia maamuzi yenye busara.
Jumiya ya Afrika Mashariki inatangazwa na viongozi lakini kila wakienda wananchi wanaikataa, sijui kuna nini hapa, hili sijalifuatilia vizuri maana lina mawazo yanayochanganya sana. Umoja tunauongelea siku zote, ingawa sio kama wa muungano wa Tanganyika na Zanzibar ambao formula yake anajua Mwl Nyerere peke yake naye sasa hayupo duniani, naona tuvute subira turekebishe mambo mengi kwanza kabla hatujaingia huko.
Blogu bado zinahitaji kudumishwa kwa nguvu zote.

Tuesday, November 07, 2006

Kikwete uso kwa uso na Al-Bashir

Wakati viongozi wa Afrika wanakutana na wenzao wa Uchina huko Beijing, China kuna mikutano mingine ya chini chini inaendelea baina ya viongozi wa nchi za kiafrika wanaohudhuria Mkutano huo mkubwa unaotarajiwa kulipatia manufaa makubwa sana bara la Afrika.
Uchina huwa haiamrishwi na Marekani na rafiki zake washirikiane na nani, hivyo maadui wakubwa wa jamii ya Marekani nao pia watahudhuria Mkutano huo mkubwa ambavyo Vyombo vya Habari(uongo!) wameanza kuutilia shaka bila ya kuwa na shaka na mambo yao wenyewe. Viongozi wa Afrika walioalikwa yumo kinara wa Afrika Raisi Bob Mugabe wa Zimbabwe aliye kwenye orodha kuu ya maadui wa magharibi, pamoja na Raisi wa Sudani Bwana Al-Bashir ambaye anasahau uafrika wake na kubariki kuangamizwa wenzake wa jimbo la Durfur kwa Sababu wao ni weusi zaidi yao! Na nywele zao ni ngumu sana!
Bila shaka, lazima Raisi wetu Mhe. J Kikwete na wenzake wengine watapata wasaha wa kukutana na Bw. Al-Bashir, na kufanya mazungumzo yaliyo au yasiyo rasmi. Ingawa kuna mambo mengi sana ya kuongelea ikiwamo ruhusa ya Tanzania kutumia maji ya Ziwa Nyanza! kukaribisha wawekezaji toka Sudan, uhusiano baina ya nchi hizi mbili. Ila bila kuongelea na ikibidi kukemea tabia au kusudi la Bw. Al-Bashir la kufumbia macho mauaji ya Durfur atakuwa hajawatendea haki watanzania na waafrika wote kwa ujumla, pia atakuwa hajatekeleza kipengele cha ilani yake ya uchaguzi aliyokuwa ameikariri kuliko misahafu kipindi cha kampeni cha kushughulikia migogoro ya jirani zetu.
Sitegemei kama kuna Mtanzania anayeunga mkono mauuaji hayo yanayoendelea kwa kasi sana, huku serikali ya sudan ikitajwa kuliimarisha jeshi la wauaji kwa kuwapatia silaha na kuzuia jeshi la nje kuingilia kati mauaji hayo.
Hivyohivyo, ingawa China ametuita kutupatia msaada naye inabidi aambiwe kwamba soko lake la silaha la Sudani linatuumiza sana kuliko hiyo misaada anayotaka kutupatia hivyo aache kuwauzia silaha wasudani na kwanza aingilie hayo mauaji ya Durfur na kuhakikisha yanakoma la siyo hiyo misaada yake haitakuwa na maana kwetu na itatuchefua zaidi kuona waafrika wanazidi kuuawa ili zipatikane pesa za kutusaidia !
Kama masuala haya pia yatakuwa agenda kwenye mkutano huo basi bara la Afrika litakuwa limetendewa haki ya kweli.